Tafuta

2025.04.25 Velatio 2025.04.25 Velatio 

Katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro ibada na kufunga jeneza la Papa Francisko imefanyika

Katika ibada fupi iliyoongozwa na Kardinali Camerlengo Farrell,baadhi ya ndugu wa Papa walikuwepo.Usiku kucha kutakuwepo na mkesha wa sala katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro.

Na Angella Rwezaula - Vatican.

Kama ilivyokuwa imetangazwa hapo awali, ibada ya kufunga jeneza la Baba Mtakatifu wa Roma imefanyika Ijumaa Aprili 25 leo usiku saa 2:00 kamili masaa ya Ulaya ikiwa ni saa 3.00 kamili saa za Afrika Mashariki na kati mbele ya Madhabahu ya Kukiri kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.

wakati wa kufunikwa
wakati wa kufunikwa   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)
Kufungwa kwa jeneza la Papa

Katika ibada iliyoongozwa na Camerlengo, wa Kanisa Takatifu la Roma, Msimamizi wa Maadhimisho ya Liturujia, Kardinali Kevin Joseph Farrell, Askofu Mkuu Diego Ravelli alisoma hati ambayo iliwekwa kwenye jeneza mwishoni mwa maadhimisho hayo.

Kubariki
Kubariki   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Mbali na yale yaliyokuwa yameoneshwa katika taarifa kutoka Ofisi ya Maadhimisho ya Liturujia za kipapa, pia baadhi ya wanafamilia wa marehemu Papa walishiriki ibada hiyo.

Kufunika vizuri
Kufunika vizuri   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Maadhimisho hayo yaliyofanyika kwa mujibu wa maagizo ya(Ordo Exsequiarum Romani Pontificis), Kanuni ya mazishi ya Papa wa Roma yalihitimishwa saa 3.00 usiku.

wakati wa kufungwa jeneza
wakati wa kufungwa jeneza   (Vatican Media)

Na wakati wote wa usiku, wajumbe wa chama cha Mtakatifu Petro watahakikisha uwepo wao kwa sala na mkesha kwa ajili ya mwili wa Papa, hadi maandalizi ya Misa Takatifu itakayofanyika kesho asubuhi tarehe 26 Aprili 2025 katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican.

Kunikwa kwa Papa na kufunga jeneza
25 Aprili 2025, 22:10