Tafuta

2025.04.26  Misa ya Mazishi ya Papa  wa Roma Francisko 2025.04.26 Misa ya Mazishi ya Papa wa Roma Francisko  (Vatican Media)

Mazishi ya Papa Francisko

Umati mkubwa unashiriki mazishi ya Papa kutoka sehemu mbali mbali za dunia.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Ni Jumamosi tarehe 26 Aprili 2025 ambapo Misa ya mazishi ya Baba Mtakatifu Francisko ikiwa inakaribia kuanza na kutangazwa na vyombo vya habari Ulimwenguni  kote kwa kuongozwa na Kardinali Giovanni Battista Re, Dekano wa Baraza la Makardinali ilisikika sauti ya kengele ya kifo.

Kuletwa kwa jeneza katika uwanja wa mtakatifu Petro

Kwa wakonselebranti karibia 5,000 wakiwemo makardinali, maaskofu, mapadre na mashemasi wanaonekana katika Uwanja wa Mtakatifu Petro. Wanashiri kwa hiyo wawakilishi kutoka watawala, kutoka makanisa ya kiekumene na dini nyingine mbali mbali za dunia, waamini wote wenye mapenzi mema kuanzia uwanja wa Mtakatifu Petro hadi mwisho wa njia ya Conciliazione!

Rangi tawala ni nyekundu
Rangi tawala ni nyekundu   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Rangi kuu katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro inayotawala ni nyekundu ya makardinali, ambao, wameingia kwa maandamano, huku wakichukua nafasi zao upande wa kushoto wakitazama Basilika, pamoja na maaskofu ndugu zao na nguo nyeusi za wawakilishi karibu 170, kutoka duniani kote wanaowakilisha nchi zao katika safu tofauti kwa upande wa kulia wa uwanja wa Mtakatifu Petro.

Jeneza likiletwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro
Jeneza likiletwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Jeneza lenye mwili wa Papa Bergoglio, lilibebwa kutoka katikati ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro wakati pembeni, kulikuwa na mistari miwili ya makardinali pande mbili, jeneza likapita katikati yao. Muda mfupi kabla, katika Basilika hiyo heshima za wakuu wa nchi  ziliendelea ikiwa ni pamoja na  rais wa Ufaransa Macron na mkewe Brigitte, William wa Uingereza na Albert wa Monaco, mfalme na malkia wa Jordan, Trump na mkewe Melania, Matarella na mtoto wake wa kike, Zelensky na wengine wengi walitoa heshima zao chini ya Madhabahu ya Kukiri, ambapo mwili wa Papa aliyekufa tangu tarehe 23 Aprili ulibaki kwa siku tatu na kuruhusu waamini wenye mapenzi mema kutoa heshima zao wakati jeneza likiwa wazi. Kwa takwimu iliyotolewa kuhusu heshima hizo, waamini karibu 250,000 walitoa heshima zao.

Mazishi ya Papa
Mazishi ya Papa   (Vatican Media)

[ Photo Embed: Wakuu wa chini na serekali mbali mbali ]

Rangi inayotawala ni nyekundu
Rangi inayotawala ni nyekundu   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Mara tu jeneza lenye mwili wa Papa Francisko lilipotokea uwanjani, yalisikia makofi ya kishindo kutoka  kwa mamia ya maelfu ya waamini waliokuwepo, huku umati ukiwa umefurika hadi njia ya Conciliazione.

Jeneza liliwekwa chini
Jeneza liliwekwa chini   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Juu ya jeneza, kama ilivyo desturi katika mazishi ya papa, iliwekwa Injili iliyofunguliwa  wazi.

 

Juu ya jeneza kuna Injili
Juu ya jeneza kuna Injili   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)
26 Aprili 2025, 10:40