Tafuta

2025.04.23 Waamini watoa heshima zao mbele ya geneza lenye mwili wa Papa Francisko. 2025.04.23 Waamini watoa heshima zao mbele ya geneza lenye mwili wa Papa Francisko.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Umati mkubwa wa waamini watoa heshima kumuaga Papa Francisko usiku kucha

Waamini waliendelea kumiminika katika kutoa heshima zao za mwisho katika Basilika ya Mtakatifu Petro kuanzia saa 5.00 asubuhi hadi saa 11.30 alfajiri na baadaye asubuhi 24 Aprili kufunguliwa tena saa 1.00.

Vatican News

Mara baada ya kuleta geneza lenye mwili wa Papa Francisko kutoka katika kikanisa cha Mtakatifu Marta mjini Vatican, Jumatano tarehe 23 Aprili 2025 asubuhi, waamini waliruhusiwa kuanzia saa 5.00 asubuhi hiyo hadi saa 11.30 alifajiri ya leo na baadaye kufungua saa 1.00 kamili. Kwa hiyo kufikia saa 2.30 asubuhi ya leo tarehe 24 Aprili watu 48,600 walitoa heshima zao kwa mwili wa Baba Mtakatifu Francisko. Usiku mzima kuanzia saa 6.00 kamili hadi saa 11.30 alfajiri waamini waliotoa heshima walikuwa ni 13,000, kwa mujibu wa taarifa.

Hata viongozi wa vyama na serikali walitoa heshima
Hata viongozi wa vyama na serikali walitoa heshima   (Vatican Media)

Rozari katika Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu

Wanafunzi wa Emau, sura zilizopotea katika giza la imani, wanakuwa uso wa Kanisa linalosonga, wakiwa wamechoshwa na uchungu na wakati mwingine hawawezi kumtambua Mfufuka wakati wa majaribu. Kardinali Baldo Reina, Makamu wa Papa Jimbo la Roma alivyoeleza jumuiya ya kikanisa iliyokusanyika katika sala ya Rozari kwa ajili ya Baba Mtakatifu Francisko, aliyerejea katika Nyumba ya Baba Jumatatu tarehe 21 Aprili 2025. Katika ukimya uliojaa kumbukumbu zinazosindikiza siku hizi, upendo wa watu wa Mungu haufifii. Unakuwa ishara, sauti, na kuwa katika sala ya Rozari. Kwenye ngazi za Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu ambapo Papa ameomba kuzikwa,  waamini walikusanyika mbele ya Salus Populi Romani, yaani Picha ya Maria iliyopendwa sana na Papa, ambayo pia usiki wa tarehe 23 Aprili waamini waliweza kusali.

Wakati wa kutoa heshima na maombi
Wakati wa kutoa heshima na maombi   (Vatican Media)

Mwanzoni mwa  matendo ya mafumbo ya utukufu ya Rozari, Kardinali Reina alisema, tukio la Pasaka linahimza kuwa maisha ni neno la mwisho  na ambalo huleta jibu jipya kwa wale wanaohoji maana ya kuteseka na kufa. Maneno ambayo huwa kubembeleza kwa watu waliochoka, moyo wa pamoja ambao kwa hakika umejaribiwa, labda kuzimwa, lakini ambao huruhusu mwanga kuchuja wakati unaruhusu kuangaziwa na imani. Picha ya Maria  Afya ya Waroma ambayo Papa alisali kabla na baada ya kila Safari ya Kitume, sasa inaalikwa kwa nguvu zaidi kuliko hapo awali. Ili maumivu haya yanaweza kubadilishwa kuwa tumaini. Kwa sababu anatukumbusha uzima na kifo sio neno la mwisho. Hata hivyo katika Basilika hiyo siku nzima, mstari katika ukimya na wa kihisia ulipitia Mlango Mtakatifu huo kama ule wa  Basilika  ya Mtakatifu Petro, kama hija ya roho kuelekea mwisho ili  kutoa heshima na kuaga Papa. 

 

 

 

24 Aprili 2025, 09:26