Kardinali Krajewski apeleka Magari manne ya kubebea wagonjwa zawadi ya Papa kwa Ukraine
Vatican News
Hali halisi ya Pasaka Mpya bado inakiwakilisha ndani ya Vita nchini Ukraine na kwa sababu hiyo Baba Mtakatifu Francisko anaendelea "kuelezea ukaribu wake kwa watu wanaoteseka kwa ishara madhubuti, miaka mitatu baada ya kumbukumbu ya uchungu na ya aibu kwa ubinadamu," kama Papa alivyokuwa amesema hapo awali.
Taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo imeripoti maneno ya Papa Francisko ya Urbi et Orbi 2024, ambayo ni chachu ya kuchukua hatua. “Ni Yesu pekee anayetufungulia milango ya uzima," Papa alisema kwamba "milango hiyo ambayo tunaifunga mara kwa mara na vita vilivyoenea ulimwenguni kote.” Hatua hiyo inahusisha kutuma Magari manne ya Wagonjwa yakiwa na nembo ya Mji wa Vatican, yenye kila chombo cha matibabu kinachohitajika kuokoa maisha ya binadamu, ambazo zitapelekwa kwenye maeneo ya vita kuwa pamoja na watu walioathirika sana na migogoro, ili kusali pamoja nao na kuwa kielelezo cha ukaribu wa Askofu wa Roma.
Kwa hiyo ni misheni ya kumi nchini Ukraine kwa Kardinali Conrad Krajewski, Mwakilishi wa Papa, misheni ambayo imezaliwa katikati ya Jubilei ya Matumaini 2025! Katika Hati ya kutangaza Jubilei Kuu ya matumaini,ya (Spes non Confundit, ya Papa Francisko anaandika kwamba: "Ishara ya kwanza ya matumaini itafsiriwe katika amani kwa ulimwengu, ambayo kwa mara nyingine inajikuta imezama katika janga la vita. Hitaji la amani ni changamoto kwa kila mtu na linahitaji kufuatilia mipango madhubuti." Zawadi ya magari 4 ya wagonjwa (ambulensi ) kwa hivyo inakuwa ishara ya tumaini la Jubilei linalojikita ndani ya Nanga ya Kristo.